Thursday, May 1, 2014

SHEREHE ZA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI "MEI MOSI" ZAFANA UWANJA WA UHURU JIJINI DAR ES SALAAM

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa kashikana mikono na viongozi wa serikali na wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) huku wakiimba wimbo wa wafanyakazi katika kilele cha Siku ya Wafanyakazi Duniani (MEI MOSI) leo Mei 1, 2014 katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. (picha: IKULU)
Rais Jakaya Kikwete, amewaahidi wafanyakazi nchini kuwa mambo mazuri yakiwemo ya kupanda kwa mishahara na kupunguzwa kwa kodi ya mishahara maarufu kama P.A.Y.E.

Akihutubia kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Dar es Salaam leo, Rais Kikwete amesema:
“Najua hiki ndio kilio chenu na wote mnasubiria kwa hamu Serikali inasema nini? Nawaahidi kuwa katika hotuba ya Bajeti Waziri wa Kazi na Ajira, itabainisha wazi, kiwango cha mshahara ambacho Serikali imekiongeza katika mishahara ya wafanyakazi,” alisema Rais Kikwete.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipungia mkono waandamanaji aliowapokea katika kilele cha Siku ya Wafanyakazi Duniani (MEI MOSI) leo Mei 1, 2014 katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


Rais Kikwete akizungumza na wafanyakazi katika sherehe za Mei Mosi katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.Rais Kikwete, alisema Serikali haitoweza kupandisha mishahara hiyo na kufikia ombi la Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA),  la Sh 750,000.

Pamoja na hayo, Rais Kikwete alionyesha kutoridhishwa na namna sehemu kubwa ya sekta binafsi, isivyozingatia viwango vya mishahara vinavyopangwa na Serikali, hali inayochangia kuibuka kwa migogoro ya mara kwa mara baina ya waajiri na waajiriwa.

Akizungumzia suala la Kodi ya Mapato (P.A.Y.E), Rais Kikwete, alisema ombi hilo nalo kama ilivyo nyongeza ya mishahara ni la muda mrefu, na kuwaahidi wafanyakazi hao kuwa nalo linafanyiwa kazi ili kupunguza kutoka asilimia 13 inayotozwa kwa sasa na kufikia tarakimu moja.

Naye Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudentia Kabaka, alimpongeza Rais Kikwete kwa kupatiwa tuzo ya utawala bora Afrika, na kuwataka waajiri nchini kutumia fursa hiyo kumuenzi kiongozi hiyo kwa kuhakikisha wanafuata nyayo na kusimamia utawala bora, ili kupunguza migogoro ya kazi.

Katibu Mkuu wa Tucta, Nicholaus Mgaya, akiwasilisha risala ya wafanyakazi katika maadhimisho hayo, aliiomba Serikali ishughulikie matatizo yanayowakabili wafanyakazi ya uboreshaji wa mishahara, kupunguzwa kwa kodi ya P.A.Y.E na kuboreshewe pensheni.Taarifa  zinasema kuwa maadhimisho hayo maarufu kama Mei Mosi yameingia dosari baada ya mmoja wa wafanyakazi kufariki dunia uwanjani kwa ghafla akiwa katika maadhimisho hayo jijini Dar es Salaam.

Mfanyakazi huyo anayedaiwa kufanya kazi Ikulu alizidiwa ghafla akiwa katika maandamano na kupatiwa huduma za kwanza lakini hali yake ilizidi kuwa mbaya na hatimaye kudaiwa kupoteza maisha wakati akipatiwa huduma na madaktari na wahudumu kutoka kikosi cha msalaba mwekundu waliyokuwa katika maadhimisho hayo.

  Mfanyakazi huyo aliletwa katika kambi ya watu wa huduma ya kwanza iliyokuwa katikati ya uwanja wa Uhuru, kisha kupatiwa huduma ya kwanza bila mafanikio na baadaye alifariki dunia. Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika kundi ambalo lilimleta mfanyakazi huyo baada ya kuzidiwa ghafla lilimtaja kuwa jina lake ni Rashid John Chilwangwa.Mmoja wa wafanyakazi waliyokuwa wameandamana na mfanyakazi huyo ambaye hakupenda kutaja jina lake kwa kuwa yeye si msemaji akisimulia tukio hilo, alisema John Chilwangwa (45) walikuwa naye katika sherehe za maadhimisho na hali yake ilibadilika kabla ya kuingia uwanjani na aliomba aende kujisaidia haja ndogo baada ya hapo alianza kuishiwa nguvu.

“…Si tulishangaa alikaa muda kidogo akijisaidia baada ya kumfuata tulimkuta ametoka ndani ya choo na kuja nje na kisha kukaa kwenye tofali huku akisema anajisikia kuishiwa nguvu na hali ilibadilika ndo tukamleta hapa,” alisema shuhuda huyo.

Alipoulizwa hali yake kwa sasa ambapo alikuwa ameingizwa kwenye hema la huduma ya kwanza kwa wahudumu kutoka kikosi cha msalaba na madaktari alisema wamejaribu kumuhudumia lakini bahati mbaya amefariki dunia tayari. 
“…Tumeambiwa na madaktari kuwa ameshafariki tayari,” alisema shuhuda huyo ambaye alikuja na mgonjwa huyo.

Mwandishi wa habari hizi alishuhudia madaktari wakijaribu kumtundikia dripu huku wakijaribu kurudisha mapigo ya moyo kwa kushtua mara kadhaa lakini juhudi ambazo hazikuzaa matunda. Baada ya kubaini amefariki dunia walisita kumwekea dripu ambayo ilikuwa inaandaliwa na badaye walimfunika kwa shuka nyeupe na kuita gari la wagonjwa tayari kwa kumpeleka hospitali kwa uchunguzi zaidi. Hata hivyo hakupatikana mara moja daktari kuzungumzia kilichomsibu Chilwangwa.
 
Baadhi ya jamaa aliyoambatana nao wakimwangalia mara baada ya kufikishwa chumba cha huduma ya kwanza. (picha: The Habari)
Rais Kikwete akifurahia jambo katika sherehe za Mei Mosi jijini Dar es salaam 
Wafanyakazi.
Mibingwa wa ligi kuu ya Vodacom 2014 Azam FC wakipita mbele ya Rais Kikwete kwenye sherehe za Mei Mosi Alhamisi 1 Mei 2014 katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.
  


WANAFUNZI WAUAWA KATIKA VURUGU ZILIZOZUKA NCHINI ETHIOPIA

Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn
Habari zinasema kumetokea vurugu za wanafunzi katika miji mbali mbali katika eneo la Oromia nchini Ethiopia.
Wakazi wa eneo la Ambo wanasema maafisa usalama walifytua risasi kwa wanafunzi ambazo zimewaua na kuwajeruhi baadhi yao.
"Wakazi wa eneo la Ambo wanasema maafisa usalama walifytua risasi kwa wanafunzi ambazo zimewaua na kuwajeruhi baadhi yao."
Ofisi ya Mambao ya Nje ya Uingereza imesema kumekuwa na hali vurugu na wasi wasi katika eneo la Ambo siku ya Jumatano.
Watu wa jamii ya Oromo hivi karibuni walikuwa wakipinga mpango kupanua mji mkuu wa Adis Ababa ambao wanasema waingilia mipaka yao.
Serikali ya Ethiopia katika siku za hivi karibuni walitia mbaroni waandishi wa habari na wafuasi wa chama kimoja cha upinzani

MSANII ABADILISHA JINA ALILOPEWA NA WAZAZI KUTOKA AZIMA MPAKA AZMA "NIA"

AZMA ni lengo, dhumuni au nia,hili ni jina lake kabisa la darasani, na ni jina ambalo alijiita mwenyewe, wazazi wake walimuita AZIMA, akiwa darasa la tatu, akajibadili na kuanza kujiita AZMA baada ya kuvutiwa na maana ya jina hilo, na akaanza kuandika AZMA badala ya AZIMA mpaka kwenye daftari la darasani.

KUWA NA AZMA au kuwa na nia,ameandika huu wimbo kama dedication kwa watu wote,wanao pambana kutafuta maisha, Maisha yana vikwazo sana,tunatapaswa kuwa na AZMA(NIA) ya dhati, katika kufanya jambo lolote, vikwazo ni sehemu ya maisha, tusikate tamaa, kwa kuwa VIKWAZO(challenges) vipo ili kuonyesha ni kiasi gani tuko STRONG. Icheck Video

KANSELA ANGELA MERKEL AANZA ZIARA YAKE NCHINI MAREKANI

Kansela Angela Merkel na Rais Obama
Kansela wa Ujerumani Angela Merkel  ameanza ziara nchini Marekani ambako amekutana na rais wa nchi hiyo, Barack Obama. Agenda ya mazungumzo yao itajikita zaidi katika mzozo wa Ukraine unaofukuta
Kansela wa Ujerumani Angela Merkel ameanza ziara  tarehe 01.05.2014 nchini Marekani ambako anatarajiwa kukutana na rais wa nchi hiyo, Barack Obama. Katika ziara yake hiyo iliyoanza jana itajikita kuongelea mzozo wa Ukraine unaofukuta utasaidia kufifisha kashfa ya kunaswa mawasiliano ya simu na kansela huyo kulikofanywa na shirika la usalama wa kitafa la Marekani, NSA.
Wakati uhusiano kati ya Urusi na mataifa tajiri ya magharibi haujawahi kuwa mbaya kama ulivyo tangu vita baridi, viongozi wa siasa na wataalamu wafikiria kuwa mzozo wa Ukraine utawafanya kuwa na msimamo mmoja baada ya miezi 6 ya mkwaruzano.
Hoja zitakazo jadiliwa na viongozi hao wawili ni mkakati wa kumshinikiza rais Vladimir Putin wa Urusi, na mkataba wa ushirikiano katika nchi za magharibi ambao umekuwa ukijadiliwa kati ya marekani na Jumuia ya Umoja wa Ulaya, alisema mshauri wa Kansela Merkel
Hii ni ziara ya kwanza ya bi Angela Merkel Washington tangu aliye kuwa mfanyakazi wa idara ya upelelezi ya Marekani Edward Snowden kutangaza kuwa kituo cha uchunguzi wa data za eletroniki cha Marekani, kimekuwa kikinasa mawasiliano ya simu Ujerumani na hususan simu ya kiganjani ya kansela.

JE MARIAH CAREY AMEWAACHIA WATOTO WAKE WACHAGUE MAADHUI YA ALBAM YAKE MPYA? ME, I AM MARIAH




Kila wakati imesemwa usijaji kitabu kwa muonekano wa picha yake lakini jina la album mpya ya Mariah Carey ni sawa ukajaji kwa cover yake ya nyuma. Kama alivyoahidi wiki iliyopita pop diva mwenye umri wa miaka 44 ametaja jina la albamu yake mpya na mchoro wa kibunifu wa kitoto na kulist majina ya nyimbo zinazopatikana ndani ya albam hiyo ikiwa ni albam yake ya 14, mchoro huo kweli unamaanisha kitu.Mashabiki wamekuwa wakiongea mambo mengi wengine wakisema muonekano na jina la albamu eti ni kwamba sasa Mariah Carey ameamua kuonyesha undani wake zaidi. Kwa nyuma ya cover inaonyesha mchoro wa kitoto na muandiko wa kitoto inamfanya mtu ajiulize kuwa amewaachia watoto wake wachague maadhui ya albam yake.Mariah Carey aliiambia Billboard kwamba ataongelea vitu vingi alivyovipitia maishani mwake katika albam hiyo mpya.. Angali hiyo video hapo chini Mariah Carey akielezea kuhusu jina la albam yake mpya ya Me, I am Mariah.

COURTNEY KOTEWA AWA MSHINDI WA SHINDANO LA "SHARE THE EXPERIENCE PHOTO"


(Picha hiyo ya juu imepigwa na Eric  Magayne)Shindano la Share the Experience photo contest limefanyika na picha iliyoshinda na kutangazwa leo ni picha iliyopigwa na mwanadada Courtney Kotewa ndani ya hifadhi ya ya taifa ya Lakeshore huko Michigani na kushinda dola 10,000. lakini picha iliyoongezewa ubunifu  ni picha iliyopigwa katika ukingo wa Ziwa Powell katika hifadhi inayoitwa Glen Canyon National Recreation Area.Picha hiyo inamuonesha mtalii akitembea katika ukingo hatari katika sehemu hiyo huko Utah, Staggs amefanya hivyo katika wakati ulio sawa akaongeza na ubunifu wake akampiga picha mtalii akitembea pembeni ya bwawa (pool) akaunganisha na sehemu ya ukingo wa Lake Powell Glen Canyon National Recreation Area. Picha hiyo ilikuwa katika shindano hilo la Share the experience photo contest 2013 ikiwa ni kati ya picha 18,000 zilizowakilishwa kwa ajili ya shindano hilo lililodhaminiwa na National Park Foundation. Picha nyingine ziangalie chini ni nzuri sana kutazama……

Picha iliyopigwa na Peter Blanchard
Picha ilipigwa na Linnea Charnholm
Picha ya Darell Staggs


Picha iliyoshinda ya mwanadada Courtney Kotewa
Picha iliyopigwa na Michal Mcruiz

Picha iliyopigwa na Graham McGeorge

JE WAJUA RYAN GIGGS ANA ASILI YA AFRICA


Ryan Giggs

Ryan Giggs alizaliwa huko Cardiff tarehe 29 Novemba 1973 kwa baba mchezaji wa zamani wa rugby Danny Wilson na mama Lynne Giggs, alipewa jina la Ryan Joseph Wilson, baada ya wazazi wake kutengana Ryan alibadili jina la ubini wake na kuitwa Ryan Giggs (jina la ubini wa mama yake) wakati huo akiwa na umri wa miaka 16.




Ryan Giggs akiwa amebebwa na baba yake Danny Wilson
Baba yake Ryan alizaliwa Wales kwa mama mwenye asili ya Wales na baba mwenye asili ya Sierra Leone (Afrika Magharibi).


Lynne Giggs (mama yake Ryan Giggs)

Ryan Giggs kulia na mdogo wake Rhodi enzi za utoto wao