Wednesday, May 21, 2014

JITIHADA ZA SERIKALI KUPAMBANA NA MIGOGORO YA WAFUGAJI NA WAKULIMA ZAANZA KUONESHA MAFANIKIO

Jitihada za Serikali na asasi za kiraia katika kuelimisha watu wa jamii ya ufugaji kutumia mifugo yao kupunguza umasikini, utunzaji wa mazingira na migogoro ya ardhi, zimeanza kuonesha mafanikio kwa baadhi ya maeneo hapa nchini.
Hali hiyo imebainika wilaya ya Manyoni mkoani Singida baada ya baadhi ya wafugaji katika eneo hilo, kuanza kuuza sehemu ya mifugo yao na kupata fedha zinazowasaidia kujenga makazi bora ya kuishi na kuwapatia elimu watoto wao.
Wakizungumza katika kijiji cha HEKA mara baada ya kutembelewa na katibu mkuu wa CCM ABDULRAHMAN KINANA, wafugaji hao wamesema hapo awali jamii hiyo ilikuwa nyuma kimaendeleo kwa kuwa hawakuelimishwa umuhimu wa kutumia mifugo katika kujikwamua kiuchumi.
Kwa upande wake katibu mkuu wa CCM komredi ABDULRAHMAN KINANA, amesema hatua hiyo imeonesha njia kwa wafugaji ambao wanajilimbikizia mifugo na kuwa watumwa wa mifugo yao.
Mkoa wa Singida una jumla ya wilaya tano na halmashauri zipatazo 6, huku asilimia 70 ya wananchi wake wakitegemea zaidi shughuli za kilimo na Ufugaji kwa ajili ya maendeleo yao.

No comments:

Post a Comment