Thursday, May 8, 2014

MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA ZAHARIBU MIUNDOMBINU WILAYANI KIBAHA

Imeelezwa kuwa mvua zinazoendelea kunyesha katika baadhi ya  maeneo hapa nchini zinazidi kuleta madhara kwa wananchi wa  Wilaya ya Kibaha, Mkoani Pwani kutokana na kuharibu miundombinu ya barabara, umeme, vyoo pamoja na kuathiri  kwa kiasi kikubwa utendaji wa kazi zao.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wananchi hao akiwemo ABDALLAH SIMBA na  KASSIM YAHAHA wamesema, madhara ya mvua hizo yamesababisha  maisha yao kuwa magumu.
Aidha wananchi hao wametoa wito kwa serikali kulitafutia ufumbuzi suala hilo, kwa kuhakikisha wanajipanga vilivyo katika kuiboresha  miundombinu ya barabara na kufanya ukarabati wa madaraja.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani HAJAT MWANTUMU  MAHIZA, ametoa tahadhari kwa wananchi kuwa makini hasa kwa wale wanaoishi katika maeneo ya mabondeni na wale wanaotumia vyombo vya baharini.
Mvua hizo zinazoendelea kunyesha katika baadhi ya maeneo zimesababisha uharibifu mkubwa wa miundombinu ya barabara, kuharibika kwa nguzo za umeme, upotevu wa mifugo pamoja na kubomoka kwa baadhi ya madaraja madogo   ambayo yalikuwa yamejengwa chini ya kiwango.

No comments:

Post a Comment