Kiongozi wa zamani wa jeshi Abdel Fattah al Sisi ameibuka na ushindi
mkubwa katika uchaguzi wa rais nchini Misri. Amejikingia zaidi ya asili
mia 90 ya kura lakini walioteremka vituoni inasemekana ni asilimia 44
tu.
Kiongozi huyo zamani wa jeshi, kwa mujibu wa duru za sheria amepata
asilimia 93 nukta 3 ya kura wakati shughuli za kuhesabu kura zikiwa
tayari zimekamilika. Mgombea Hamdine Sabahi, mpinzani pekee katika
uchaguzi huo amepata asilimia 3 nukta 8 ya kura, huku asilimia 3 nukta 7
ya kuwa ikiwa ni kura zilizoharibika.
Lakini idadi ya walioshiriki kupiga kura ikadiriwa asilimia 44 nukta 4,
kwa mujibu wa duru hizo na hivyo kuweka shaka kwenye uhalali wa Al-
Sisi, muasisi wa mapinduzi yaliyomuondowa madarakani Julai mwaka jana
rais aliyechaguliwa kidemokrasia Mohamed Morsi.
Yalipoanza kutangazwa matokeo ya uchaguzi, wafuasi wa Al Sisi
walizunguka barabara za Cairo na kupeperusha bendera wakisheherekea
ushindi wa mgombea wao, huku honi za gari zikisikia katika mji mkuu.
Usiku kucha wafuasi hao wa Jemedari mstaafu Sisi walijumuika wakiimba na
kucheza kwenye eneo maarufu la Tahrir lililoshuhudia maandamano makubwa
yaliyompinduwa aliyekuwa rais wa Msri, Hosni Mubarak Novemba 2011,
baada ya kuiongoza Misri kwa zaidi ya miaka 30.
No comments:
Post a Comment