Monday, May 12, 2014

KATIBU MKUU WA CCM AWATAKA WANANCHI KUWA MAKINI DHIDI YA WANASIASA WANAOSEMA KATIBA MPYA NDIO SULUHU YA MATATIZO YAO

Katibu mkuu wa chama cha Mapinduzi, komredi ABDULRAHMAN KINANA amewataka wananchi kuwa makini dhidi ya wanasiasa wanaopita mitaani na kudai kuwa upatikanaji wa katiba mpya ndio suluhu ya matatizo yao.
Amesema kauli mbalimbali zinazoendelea kutolewa na baadhi ya wanasiasa nchini kuhusiana na suala la muungano na muundo wa Serikali tatu ndani ya katiba ijayo, zina lengo la kutaka kujilimbikizia madaraka na vyeo ambavyo kimsingi havina tija kwa maslahi ya Watanzania.
Akizungumza katika mkutano wake na wananchi wa Jimbo la BUKENE, wilaya ya NZEGA mkoani TABORA mara baada ya kukagua miradi ya maendeleo, katibu mkuu huyo wa CCM amesema wanasiasa hao walipokuwa katika vikao vya bunge la katiba mjini Dodoma wameonekana kutetea maslahi yao zaidi kuliko haki za wananchi wa kawaida.
Katika hatua nyingine Mbunge wa jimbo la Bukene SULEYMANI ZEDI alizungumza katika mkutano huo, amesema Serikali imefanikiwa kutimiza ahadi ya kupeleka umeme katika jimbo hilo, ingawa bado kuna changamoto kubwa ya kukosekana kwa nguzo.
Ziara ya katibu mkuu wa CCM, bado inaendelea mkoani Tabora ambapo baadae ataelekea mkoani Singida kwa ajili ya kuangalia utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya chama hicho ya mwaka 2010.

No comments:

Post a Comment