Friday, May 23, 2014

DAR ES SALAAM INAONGOZA KWA WATU WENGI KWA MUJIBU WA SENSA YA WATU NA MAKAZI YA MWAKA 2012

Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 nchi ya Tanzania ina zaidi ya watu Milioni 44, ambapo Mkoa wa Dar es Salaam unaongoza kuliko mikoa yote nchini, wenyewe ukiwa na watu wanaofikia milioni 4.3.
Licha ya takwimu hizo kuonesha ongezeko hilo la watu kutoka Milioni 36 mwaka 2002 hadi kufikia Milioni 44.5, tafiti zinaonesha kuwepo kwa watoto wengi wanaoishi kwenye mazingira magumu, kwenye Wilaya 108 nchini mwaka 2012/  2013 ambapo Wavulana ni 474, 424 sawa na asilimia 53 huku Wasichana  wakiwa 420, 424 sawa na asilimia 47.
Kutokana na changamoto hiyo imebainika kuwa kati ya watoto hao, zaidi ya 70 miongoni mwao wanaishi katika kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi Ubungo na kukutana na kiongozi wao anayefahamika kwa jina maarufu RAMA FUNDI.
Sheria ya Haki za Mtoto iliyotafsiriwa mwaka 2009 inabainisha masuala mbalimbali ikiwemo mtoto kutotengwa, kujua jina au utaifa wake, kuishi na wazazi ama walezi ikiwemo wajibu wa kumtunza mtoto, kama ilivyo sheria ni msumeno,  je watoto hao wanazijua haki zao ili kuweza kukabiliana na matatizo wanayokumbana nayo? 
Dawati la Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu LHRC lililo chini ya Ofisa Mradi wake Wakili NAEMI SILAYO lina wajibu wa kuhakikisha haki za watoto hazipindishwi, kama sheria ya watoto ya mwaka 2009 inavyobainisha.
Serikali kupitia Maafisa Watendaji nao kwa nafasi zao wanawajibika kuhakikisha watoto katika maeneo yao wanapatiwa haki zao ikiwemo ya kucheza na kufurahia maisha, je nao wamechukua juhudi zozote katika kuwasaidia watoto hao.
Mke wa Rais Mama SALMA KIKWETE amewahi kusema, MTOTO WA MWENZIO NI WAKO UMLINDE, je umeshawahi kuchukua juhudi zozote za kuwalinda watoto wanaonyanyaswa katika jamii yako, kama bado chukua hatua.

No comments:

Post a Comment