Thursday, May 8, 2014

KATIKA KUKABILIANA NA UHARAMIA NA UTEKAJI WA MALI ZA WAVUVI ZIWA TANGANYIKA IDARA YA UHAMIAJI YATAKIWA KUANGALI UPYA UTOAJI WA VIBALI

Ili kukabiliana na uharamia na utekaji wa mali za wavuvi unaofanywa kwenye ziwa Tanganyika, Mkuu  wa mkoa wa Kigoma ISSA MACHIBYA, ameitaka idara ya uhamiaji mkoani humo kuangalia upya taratibu za  utoaji wa vibali vya kazi ,na vibali vya kuishi, kwa watu kutoka nchi za maziwa makuu ambao wanaajiriwa kufanya kazi za uvuvi mkoani Kigoma.
Akikabidhi mashine nne za boti ambazo zimefanikiwa kuokolewa kutoka mikononi mwa majambazi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) mwanzoni mwa wiki hii, MACHIBYA amesema uchunguzi unaonyesha kuwa vitendo vya utekaji wa mali za wavuvi katika ziwa Tanganyika kwa kiasi kikubwa umekuwa ukifanywa na watu kutoka nchi nchi hiyo na Burundi.
Kufuatia hali hiyo, mwenyekiti wa chama cha wavuvi mkoani Kigoma RAMADHANI KANYONGO amesema, mali zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni tano zimeporwa mkoani humo, katika kipindi cha miaka 10 iliyopita.
 Akitoa taarifa kuhusu tukio lililotokea mwishoni mwa wiki iliyopita, Kamanda wa polisi mkoa wa Kigoma FRAISSER KASHAI amesema, jumla ya boti moja na mashine saba za boti zilitekwa, ambapo nahodha wa boti iliyotekwa alifanikiwa kuwatoroka majambazi hayo kutoka mkoa wa KALEMIE nchini DRC na kufanikiwa kurudi na mashine nne za boti ,ambazo zilikuwa sehemu ya vifaa vilivyotekwa katika tukio hilo.
Kufuatia kitendo hicho cha kishujaa, mbali na kumkabidhi fedha taslimu, Mkuu wa wilaya ya kibondo, VENANCE MWAMOTTO
Amemsifia nahodha huyo kwa kitendo chake cha ujasiri.

No comments:

Post a Comment