Monday, May 19, 2014

SHIRIKA LINALOWASAIDIA WAZEE WILAYANI KARAGWE LAANZA KUTEKELEZA MIKAKATI YAKE

Shirika lisilo la kiserikali linalowasaidia wazee wilayani Karagwe (SAWAKA) limeanza kutekeleza  mikakati yake yenye lengo la kupunguza kasi ya  vitendo vya ukatili na manyanayaso dhidi ya wazee wanayokumbana nayo katika jamii.
 Akizungumza wakati wa warsha maalumu iliyoandaliwa na shirika hilo Mkurugenzi Mtendaji wa SAWAKA LIVINGSTONE BYEKWASO amesema shirika limeanza kuwawezesha wazee kiuchumi ili waweze kujiongezea kipato.
 Nao baadhi ya wanahabari waliohudhuria warsha hiyo akiwemo LILIAN LUGAKINGIRA, MBEKI MBEKI na AGNES DAMAS kwa nyakati tofauti wameishauri serikali kubuni mikakati mbalimbali itakayochangia kukomesha kabisa vitendo vya ukatili  na manyanyaso wanayokumbana nayo wazee.
Tangu lianzishwe shirika hilo mwaka 2005 limeshawajengea wazee nyumba zaidi ya MIA MBILI TISINI na MOJA.

No comments:

Post a Comment