Wednesday, May 21, 2014

SUALA LA ELIMU NI JUKUMU LA JAMII NZIMA - ABBAS KANDORO

Walimu na wadau wa elimu mkoani Mbeya wameitaka Serikali kutoa elimu kwa jamii juu ya mpango wa matokeo makubwa BRN ili mpango huo uweze kuleta tija.
Wakizungumza katika hafla ya kukabidhi vyeti kwa shule ambazo zimeongeza ufaulu kwenye mitihani ya kitaifa mkoani Mbeya, baadhi ya walimu wamesema bado kuna changamoto kubwa ya jamii kutoelewa malengo ya mpango huo,kiasi cha baadhi ya wazazi kutotoa ushirikiano katika maendeleo ya taaluma kwa watoto wao.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro amesema suala la maendeleo ya taaluma mkoani Mbeya ni jukumu la jamii nzima, hivyo ni muhimu kwa wazazi na walimu kushirikiana katika kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu  bora
Mkoa wa Mbeya ni miongoni mwa mikoa ambayo imefanya vizuri kitaaluma katika mwaka wa masomo wa 2013/2014 ukishika nafasi ya tatu katika mikoa yote ya Tanzania bara sambamba na kutoa shule iliyoongoza kitaifa kwenye matokeo ya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2013.

No comments:

Post a Comment