Friday, May 23, 2014

SERIKALI IMETAKIWA KUWEKA MIPANGO YA MATUMIZI BORA YA ARDHI

Serikali imetakiwa kuweka mipango ya matumizi bora ya ardhi kwa kutenga maeneo ya wakulima na wafugaji ili kuepusha migogoro ya mara kwa mara ya wakulima na wafugaji, ambayo imekuwa ikisababisha vifo vya wananchi na mifugo katika maeneo mbalimbali nchini.
Rai hiyo imetolewa na Kamati ya Bunge ya kilimo, mifugo na maji kupitia kwa mwakilishi wake AMINA MAKILAGI na Kambi Rasmi ya upinzani bungeni kupitia kwa Waziri Kivuli wa Mifugo na Uvuvi ROSEMARY KAMILI wakati wakitoa maoni kwa makadirio ya mapato na matumizi ya wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2014/2015.
Pamoja na rai, suala na kuiwezesha sekta ya mifugo kuchangia pato la Taifa limezungumziwa, huku Kambi rasmi ya upinzani bungeni ikitaka kuwasilishwa bungeni kwa taarifa ya uchunguzi ya kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira kuhusu migogoro ya wakulima, wafugaji na hifadhi, huku wakitaka kufutwa kwa kodi ya mifugo.
Awali akiwasilisha hotuba ya makadirio ya bajeti ya Wizara yake kwa mwaka 2014/2015 suala la oparesheni tokomeza, waziri wa Mifugo na Uvuvi Dk. TITUS KAMANI ameahidi kutenga maeneo maalum kwa ajili ya wafugaji ikiwa ni sehemu ya kupunguza migogoro baina ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi huku akibainisha kuwepo kwa ongezeko la uzalishaji wa nyama.
Tanzania ina jumla ya Ngombe milioni 22.8, Mbuzi milioni 15.6, Kondoo milioni 7, Nguruwe milioni 2.01, Kuku wa Asili milioni 35.5 na Kuku wa kisasa milioni 24.5.

No comments:

Post a Comment