Monday, May 12, 2014

MAKUBALIANO YA AMANI YAVUNJWA NCHINI SUDAN

Vikosi vya serikali ya Sudan Kusini na waasi wanaendelea kupigana wakivunja makubaliano mapya ya amani na kuondoa matumaini ya kumaliza miezi mitano ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Mapigano yamepamba moto katika jimbo tajiri kwa mafuta la Nile ya juu,kwa mujibu wa waziri wa ulinzi Kuol Mayang aliyesema vikosi vya serikali vimeamariwa" visende kupigana,lakini vijihami tu vikishambuliwa."

Tangu rais Silva Kiir na kiongozi wa waasi Riek Machar walipotia saini makubaliano ya kuweka chini silaha ijumaa iliyopita,pande zote mbili zinaendelea kulaumiana kuanzisha upya mashambulio .
"Riek Machar havidhibiti vikosi vyake na wanamgambo wake wenye silaha nzito nzito wanaojulikana kama "Jeshi jeupe" wanaojipakaa jivu kama alama ya vita na wakati huo huo kuepusha wasitafunwe na mbu" wamewashambulia wanajeshi wa serikali,waziri wa ulinzi Manyang ameendelea kusema.

"Hivi si vikosi vya kawaida,jeshi jeupe limeundwa na raia na hawajaarifiwa chochote kuhusu makubaliano yaliyofikiwa ili kusitisha uhasama-waziri huyo wa ulinzi wa serikali ya mjini Juba amesema na kuongeza waasi ndio waliokuwa wa kwanza kushambulia.
Nae msemaji wa jeshi Philip Aguer amesema wasimamizi kutoka jumuia ya IGAD wanapelekwa Bentiu,mji mkuu wa jimbo tajiri kwa mafuta Unity .
Rais Salva Kiir amesisitiza alipokuwa akiuhutubia umati wa watu huko Juba kwamba anataka amani."Tumewaamuru wanajeshi wetu wasibanduke mahala walipo kuwashambulia waasi."Amesema.

Pande hizi mbili ziliwahi kukubaliana kuweka chini silaha mwezi january uliopita,lakini makubaliano hayo hayakukawia kuvunjika na wimbi jipya la mapigano kuripuka.
Wachunguzi wa mambo wanasema pande zote mbili zinakabiliwa na changamoto ya jinsi ya kutekeleza makubaliano ya amani huku muungano wa makundi ya wanamgambo yakiwaleta pamoja wanajeshi walioasi na makundi yanayohasimiana ya kikabila.

Pande zote mbili zinalaumiana kuwatumia mamluki na waasi kutoka nchi jirani ya Sudan huku upande wa serikali ukiungwa mkono na wanajeshi wa Uganda-Muundo wa Uongozi wa Kiir unatajikana pia kuwa dhaifu.

No comments:

Post a Comment