Uchina imeanza kulegeza sheria zake za mpango
wa uzazi, na sasa inapiga kampeni ya kuongeza angalau watoto millioni mbili
zaidi wanaozaliwa kila mwaka.
Serikali itaongeza wakunga na wahudumu sambamba
na kupanua nafasi hospitalini na kuongezwa idadi ya vitanda na vifaa
vinginevyo.
Kwa muda mrefu Uchina imeendeleza sera kali ya
mpango wa uzazi ya kulazimu familia kuwa na mtoto mmoja tu, huku wanaokiuka
wakichukuliwa hatua kali jambo linaloshutumiwa kimataifa.
Lakini mwaka jana serikali ilianza kulegeza
kamba kwa kusema iwapo mmoja wa wazazi amekuwa mtoto wa pekee katika familia,
basi anaweza kuzaa mtoto wa pili.
Japo hatua za awali zilichukuliwa kukabiliana
na idadi kubwa ya watu nchini humo, sasa kumetokea mapungufu ambayo yanahitaji
kusawazishwa.
Nao Wapanga sera wamependekeza juhudi hizo za
kuongeza idadi ya watoto, zichukuliwe sasa la sivyo Uchina itajikuta na
upungufu mkubwa wa nguvu kazi za vijana, huku idadi ya wazee na wanaostaafu
ikiwa kubwa kiasi cha kuzorotesha uchumi wa taifa hilo kubwa duniani.
No comments:
Post a Comment