Monday, May 5, 2014

KINANA AMTAKA MAALIM SEIF AJIUZULU



Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akihutibia wananchi katika uwanja wa Kibandamaiti Zanzibar.
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) kimemtaka Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Seif Sharif Hamad kama kweli hataki Muungano wa serikali mbili amuandikie barua Rais wa Zanzibar, Dk Mohamed Shein na kujiuzulu wadhifa wake wa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar. 

Tamko hilo lilitolewa jana na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana wakati akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kibandamaiti mjini Unguja. Kinana alisema anachokifanya Seif ni sawa na kuwaramba visogo wanasiasa wenzake wa upinzani, wakati yeye akipata mshahara na marupurupu mengine yanayomwendesha maisha yak echini ya serikali ya CCM.

 Alisema kama kweli Maalim Seif anajigamba ni jasiri achukue uamuzi sahihi wa kujiuzulu wadhifa wake ili apate nafasi ya kutosha kuwatumikia wananchi nje ya Serikali. Kinana alieleza kuwa kutembea nchi nzima kwa Seif si kitendo cha uungwana kufanywa na kiongozi mwenye wadhifa wa Makamu wa kwanza wa Rais akiwa ndani ya Serikali inayompa mshahara na huduma nyingine muhimu akaamua kuwachcochea wenzake ambao wako nje ya Serikali kuleta chokochoko dhidi ya Serikali anayoitumikia. Maalim Seif ameshatuhumiwa kuwa kigeugeu katika maisha yake ya kisiasa ambapo hivi karibuni Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Mohammed Seif Khatib alielezea namna kiongozi huyo wa CUF alivyowahi kuwa mtetezi wa serikali mbili alipokuwa kiongozi katika Serikali ya CCM ambako alitumia nguvu kubwa kupinga vuguvugu la kudai serikali tatu mwaka 1984.Khatibu alinukuu kauli ya Maalim Seif alipokuwa akipambana na watu waliokuwa wakaitaka serikali tatu akiwemo Rais wa Zanzibar wakti huo Aboud Jumbe. 

“Msimamo wa Jumbe umetufadhaisha sisi sote tunataka maelezo yake kwa kuwa ni dhahiri hoja ya serikali tatau haikuanzishwa na watu wadogo, imechangiwa pia na baadhi ya viongozi wa Baraza la Mapinduzi na Aboud Jumbe ni chanzo cha hayo” alinukuliwa Maalim Seif akisema mwaka 1984. Viongozi ambao Maalim Seif alisema wnataka serikali tatu na kwa kufanya hivyo wamemfadhaisha na wanastahili adhabu pamoja na Jumbe ni Jamal Faki, Abuu Salim na Wolfgang Dourado ambaye alikuwa mwanasheria Mkuu wa kwanza wa Zanzibar. 

“Tuangalie viongozi wanaobadilikabadilika mwaka 1984 Maalim alitaka serikali mbili, mwaka 1992 akiwa CUF msimamo wake ukawa serikali tatu, juzi serikali ya mkataba, huyu ni kiongozi wa aiana gani? Ni wa kuongopea watu tu”. Alisema Khatibu Aman nia mbaya Kinana katika mkutano wa jana aliendelea kusema. “Maalim Seif aache kuwababaisha wananchi atulie kwa sababu ameamua kutumikia serikali za CCM na hana uwezo wowote wa kuvuruga amani ya Taifa kama anavyojigamba kwenye majukwaa ya kisiasa. 

 Aliongeza kuwa Katibu Mkuu huyo wa CUF anaposimama na kutaka muundo wa Muungano wa serikali tatu hiyo ni danganaya toto lakini kila mwenye macho na amasikio anatambua nia ya kiongozi huyo ni kutaka kuusambaratisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa maslahi yake na rafiki zake. Kinana alisema Tanganyika kukosa Serikali wakati Zanzibar ikiwa na mamlaka ya ndani si kioja kwani hata Uingereza yenye Muungano wa nchi za Wales, Scotland, Ireland ya Kaskazini na England ina kiti kimoja Umoja wa mAtaifa. 

Pia alisema England ambako anatoka Malkia Elizabeth II haina serikali. Kwa upande wake Mnadhimu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Salmin Awadh Salmin alisema wawakilishi wa CCM wanatazamia kuwasilisha hoja binafsi kwenye Baraza la Wawakilishi Zanzibar ili wananchi waulizwe kama wanaafiki mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa visiwani humo au la. Salmin alisema dhamira na madhumuni ya kuundwa kwa serikali ya Umoja wa Kitaifa imefutika na haileti tena matumaini kwa wananchi kwa kuwa pande mbili za kisiasa zinazounda ushirika huo zina itikadi zinazotofautiana.

No comments:

Post a Comment