Wednesday, May 21, 2014

MIAKA 18 TOKA ILIPOZAMA MELI YA MV BUKOBA

Alfajiri ya Mei 21 mwaka 1996 ni siku itakayobaki kwenye kumbukumbu ya Watanzania baada ya watu zaidi ya 800 kufariki dunia kufuatia Meli ya MV Bukoba waliyokuwa wakisafiria kutoka mkoani Kagera kuelekea Mwanza kuzama katika Ziwa Victoria.
Tukiadhimisha miaka 18 tangu kutokea kwa ajali hiyo iliyokatisha maisha ya wapendwa wetu, taifa leo linakumbuka simanzi kutokana na kupoteza ndugu, uhai wa watu hao, ikiwemo mchango wao katika kuliletea taifa maendeleo.
Wakati ajali hiyo inatokea Rais Mstaafu  wa Awamu ya tatu BENJAMIN WILLIAM MKAPA alikuwa madarakani.
Ajali za majini zimeendelea kutokea ambapo Septemba 10 mwaka 2011 Meli ya Spice Islander ilizama katika eneo la Nungwi ikitokea Bandari ya Malindi Zanzibar na kuua zaidi ya watu 100.
Mwaka mmoja yaani Julai 18 2012, baadae karibu na Pwani ya Zanzibar Meli ya MV Skagit iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kwenda Zanzibar ilizama na kuua abiria 146 kati ya 290 waliokuwa kwenye meli hiyo.
Mara nyingi binadamu hujifunza kutokana na makosa, ambapo ajali hizi mara nyingi zinadaiwa kusababishwa na uzembe wa baadhi ya watendaji na watoa huduma
Aidha jamii imeitakiwa  kwa ujumla kuimarisha usalama katika usafiri wa majini na sio kuiachia mamlaka husika pekee.

No comments:

Post a Comment