![]() |
Mhe. Samia Suluhu Hassan |
Tanzania ni
miongoni mwa nchi zinazoathiriwa na mabadiliko ya tabianchi ambayo yamekuwa
yakisababisha kuwepo kwa mvua nyingi pamoja na ukame katika baadhi ya maeneo.
Ili kukabiliana
na athari za mabadiliko ya Tabianchi, Waziri wa nchi ofisi ya makamu wa Rais
Mazingira SAMIA SULUHU HASSAN,wakati akiwasilisha bajeti ya Ofisi ya Makamu wa
Rais kwa mwaka wa fedha 2014/2015,amesema wamepunguza gharama za nishati
mbadala kwa asilimia 18 ya kodi ya ongezeko la thamani kwa vifaa vya uzalishaji
wa nishati za upepo na gesi.
Kwa upande
wa kamati ya Katiba, sheria na utawala, mwakilishi wa kamati hiyo FAHARIA
SHOMARI, amesema wananchi wengi bado hawafahamu faida ya muungano na mgawanyo
wa mapato huku mwakilishi wa kamati ya Maliasili na Mazingira ALSHAIMAA QWEGIR
akiitaka Serikali kuvunja nyumba zote zilizojengwa kwenye hifadhi za mito,
maziwa na bahari.
Katika hatua
nyingine Kambi rasmi ya upinzani Bungeni kupitia kwa msemaji wake wa Katiba na
Sheria TUNDU LISSU imehoji kutolewa kwa mapato pungufu kwa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar kinyume na taratibu.
Tukisalia
bungeni mbunge wa Kigamboni Dk. FAUSTIN NDUGULILE nae ameitaka Wizara ya Afya
na Ustawi wa Jamii kuwasilisha bungeni taarifa ya Ugonjwa wa Homa ya Dengu,
Dalili zake na hatua zinazochukuliwa na Serikali mpaka sasa ili kuwatoa hofu
wananchi jambo ambalo limeungwa mkono na Mwenyekiti wa Bunge MUSSA AZAN ZUNGU.
No comments:
Post a Comment