Wednesday, May 7, 2014

MIKOA YA MWANZA NA IRINGA INAKABILIWA NA CHANGAMOTO KWA WANANCHI WAKE KUSHINDWA KUTAMBUA DALILI ZA AWALI ZA MAGONJWA YASIYOPEWA KIPAUMBELE

Mikoa ya MWANZA na IRINGA bado inakabiliwa na changamoto ya wananchi wake kushindwa kutambua dalili za awali za magonjwa yasiyopewa kipaumbele, huku zaidi ya watu bilioni mbili wakiwa hatarini kupata maambukizi ya magonjwa hayo.
Kwa mujibu wa ripoti na tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa maambukizi ya magonjwa yasiyopewa kipaumbele ikiwemo usubi, matende, ngirimaji, minyoo ya tumbo, kichocho na trakoma yametajwa kuathiri kwa kiasi kikubwa jamii maskini.
Wakizungumza jijini Dar es Salaam, waratibu wa magonjwa hayo kutoka mikoa ya Mwanza na Iringa wamesema elimu ya ufahamu wa dalili za mapema za maradhi hayo inahitajika kutolewa hasa ikizingatiwa kuwa athari zake ni ulemavu wa kudumu.
Katika kukabiliana na athari za magonjwa hayo Serikali kupitia wizara ya Afya na ustawi wa Jamii imekuwa ikipanga mikakati mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanakuwa na uelewa wa kutosha.

No comments:

Post a Comment