Na goli la pili la Manchester City lilifungwa Kapteni wa timu Vicent Kompany katika dakika 49 dakika tano tu baada ya kipindi cha pili kuanza na kuiweka Man City sehemu salama katika kuwa bingwa wa Uingereza kwa mara ya pili ndani ya misimu mitatu. Baada ya kipenga cha mwisho mashabiki wa Man City waliingia uwanjani kwa furaha kuwafuata wachezaji ni kufanya uwanja wote kujaa mashabiki katika sehemu ya kuchezea (pitch). Mechi nyingine ilikuwa ni Liverpool dhidi ya Newcastle na Liverpool ameshinda 2 – 0 na kukamata nafasi yake ya pili kwa tofauti ya pointi 1 alizotofautiana na bingwa Man City mwenye pointi 86.
Mechi nyingine kwenye ligi zilizochezwa leo ni Cardiff 1 – 2 Chelsea, Fulham 2 – 2 Crystal Palace, Hull 0 – 2 Everton, Liverpool 2 – 1 Newcastle, Man City 2 – 0 West Ham United, Norwich 0 – 2 Arsenal kutokana na kufungwa kwa Norwich ndo tiketi yake ya kushuka daraja. Southampton 1 – 1 Man United, Sunderland 1 – 3 Swansea, Tottenham 3 – 0 Aston Villa na West Brom 1 – 2 Stoke. Timu nyingine zilizoshuka daraja ni Norwich na Fulham.Mfungaji bora wa ligi hiyo ni Suarez mwenye magoli 31, Sturridge 21 wote wachezaji wa Liverpool, nafasi ya tatu kwa ufungaji inashikiliwa na Yaya Toure wa Man City ana magoli 20, Aguero wa Man City na Rooney wa Man United wamelingana kwa magoli kila mmoja ana magoli 17.
No comments:
Post a Comment