Tuesday, May 6, 2014

WANANCHI WILAYANI MKALAMA SINGIDA WAMEOMBA KUPUNGUZWA KWA URASIMU KATIKA UTOAJI WA VYETI



Baadhi ya wananchi wa wilaya ya Mkalama Mkoani Singida wameiomba ofisi ya usajili wa vizazi na vifo Wilayani humo, kupunguza urasimu juu ya upatikanaji wa vyeti baada ya malipo.
Wakiongea kwenye mkutano wa baraza  la madiwani, baadhi ya madiwani akiwemo ABDALAH MKILYA wamesema licha ya ucheleweshaji huo, pia vinauzwa kwa gharama ya Shilingi elfu 10 badala ya shingi elfu mbili kama ilivyoainishwa kwenye risiti.
Akijibu malamamiko hayo, katibu tawala wa wilaya hiyo Benjamin Mwombeki amesema kiasi cha fedha kinachotozwa sasa kipo kisheria, isipokuwa stakabadhi zinazotumika zinaonyesha kiwango cha zamani.
Aidha katika hatua nyingine madiwani hao wameiomba serikali ya Wilaya hiyo kutafuta ufumbuzi wa tatizo la mipaka kati ya wilaya yao na Mbulu, Hanang, Karatu, Iramba, na Singida vijijini, pamoja na  mipaka ya ndani baina ya kata na kata.

Halmashauri ya Wilaya Mkalama ni kati ya Wilaya mpya nchini, zilizoanzishwa na kupata hadhi kamili ya kuwa Wilaya.

No comments:

Post a Comment