Kauli hiyo
imekuja kufuatia hoja iliyotolewa na Diwani wa kata ya Msangani LEONARD
MLOE katika kikao cha baraza la madiwani ambaye alitaka ufafanuzi kuhusu ujenzi
wa zahanati hiyo ambayo imemalizika kwa muda mrefu lakini
haijaanza kutumika.
Akijibu
hoja hiyo,mwenyekiti huyo wa halmashauri amesema hakuna sababu yoyote ya
zahanati hiyo kushindwa kuanza kufanya kazi ukizingatia mambo yote muhimu
yameshakamilika ikiwemo nyumba ya daktari.
Hoja hiyo ya
sakata la kufunguliwa kwa zahanati imeonekana kuwakera viongozi
waliohudhuria kikao hicho hali iliyomlazimu mwenyekiti wa Chama cha
mapinduzi CCM Wilayani Kibaha MAULID BUNDALA kusimama na kueleza kusikitishwa
na kutokufunguliwa kwa zahanati hiyo wakati ipo tayari.
Wakazi wa kata
ya msangani wanalazimika kutembea umbali wa zaidi ya kilomita 10 kufuata
huduma za afya katika kata
ya mwendapole kutokana na kukosa huduma hiyo kwenye kata yao.
No comments:
Post a Comment