Tuesday, May 20, 2014

VAN GAAL MENEJA MPYA WA MANCHESTER UNITED



Klabu ya Manchester United imemteua Lous Van Gaal kuwa kocha wake mpya atakayechukua nafasi baada ya David Moyes kutimuliwa kwa miezi 10 tu. Mholanzi huyo amesaini mkataba wa miaka mitatau na ataanza majukumu Old Trafford msimu unaokuja ikiwa ni baada kuongoza timu ya nchi yake Uholanzi katika kombe la dunia litakalofanyika nchini Brazil. Msaidi wa Van Gaal atakuwa Ryna Giggs mkongwe wa klabu hiyo ambayo alitwa majukumu ya kuiongoza Man U baada ya Moyes kufukuzwa zikiwa zimebaki mechi tatu msimu kukamilika. Van Gaal mwenye umri wa mika 62 amewahi kuzifundisha klabu za Ajax (Uholanzi), Barcelona (Uhispania) na Bayrn Munich (Ujerumani) ambazo aliziwezesha kushinda mataji ya Ligi Kuu kabla ya kuajiriwa kuiona kikosi cha taifa cha Uholanzi maarufu kama “Orange”.

Kocha huyo anategemewa kufufua matumaini ya United baada ya klabu hiyo kumaliza ya saba msimu huu chini ya Moyes na kuandikisha historia ya kuwa na msimu mbaya zaidi kwa kipindi cha miaka 24. Van Gaal alishinda mataji mawili ya La Liga akiwa na Barcelona na kujiunga na Bayern aliyotwaa nayo kombe la German Cup na kufika fainali Uefa. Alijizolea umaarufu mwaka 1995 baada ya kukiongoza kikosi kichanga cha Ajax kilichokuwa na Clarence Seadoff, Patrick Kluivert na wengine na kutwa kombe la Uefa kwa kuilaza AC Milan ya Italia.

No comments:

Post a Comment