Thursday, May 29, 2014

Serikali Yatakiwa Kufanyia Kazi Marekebisho Sheria Ya Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa

Serikali imetakiwa kukamilisha taratibu zote muhimu, ikiwemo kuifanyia marekebisho sheria ya uchaguzi wa Serikali za mitaa, ili kuepusha dosari zilizojitokeza katika uchaguzi uliopita.
Rai hiyo imetolewa na kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni FREEMAN MBOWE, wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu MIZENGO PINDA ambaye amesema, hatua iliyoanza ni maandalizi ya bajeti huku taratibu zikifanyika, kuangalia maeneo yote muhimu yakiwemo yanayolalamikiwa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Mbunge wa Kilwa MURTAZA MANGUNGU amemtaka Waziri Mkuu kuingilia kati, mkanganyiko wa uongozi katika jiji la Dar es Salaam kuhusu suala la uchafu uliokithiri jijini humo, kunakotokana na Halmashauri kuacha baadhi ya majukumu kwa kisingizio kuwa ni jukumu la jiji, jambo ambalo Waziri Mkuu MIZENGO PINDA ameshauri lianzie katika ngazi ya chini.

No comments:

Post a Comment