Monday, May 19, 2014

CHAMA CHA MAPINDUZI KIMEDAI KUFADHAISHWA NA NA UTENDAJI MMBOVU WA WATENDAJI WA SERIKALI

Chama mapinduzi CCM kimedai kufadhaishwa na utendaji mbovu wa watendaji wa Serikali katika baadhi ya Halmashauri nchini.
Kimesema utendaji huo mbovu ni pamoja na kutowawajibisha kwa manufaa ya umma, kama ilivyokua enzi za utawala wa hayati mwalimu JULIUS KAMBARAGE NYERERE na mwenzake AMANI ABEID KARUME.
Akihitimisha ziara ya siku 11 mkoani TABORA katibu mkuu wa CCM, ABDULRAHMAN KINANA, amesema mateso wanayopata wananchi hivi sasa yametokana na baadhi ya viongozi wa Serikali kutojali kuwatumikia wananchi huku wakiikandamiza dhana nzima ya utawala bora.
Kwa Upande wake katibu wa NEC itikadi na Uenezi NAPE NNAUYE amedai kushangazwa na hoja za baadhi ya makundi ya wanasiasa yanayodai kuwa ziara za katibu mkuu wa chama hicho zimelenga kuzungumzia suala la katiba pamoja na Ukawa.
Katibu mkuu huyo wa CCM, mara baada ya kuhitimisha ziara yake mkoani Tabora,ameelekea Singida kuangalia kero na matatizo ya wananchi ikiwa ni muendelezo wa ziara yake.

No comments:

Post a Comment