Tuesday, May 6, 2014

BUNGE LAVUNJA KANUNI ZAKE ILIZOJIWEKEA KATIKA KUENDESHA VIKAO ILI KUKAMILISHA KWA WAKATI MKUTANO WA BUNGE LA BAJETI



Bunge la Tanzania hatimaye limeridhia kuzivunja kanuni zake
ilizojiwekea katika kuendesha vikao mbalimbali ili kuwezesha
kukamilisha kwa wakati mchakato wa mkutano wa Bunge la Bajeti ya Serikali mwaka 2014/2015 unaotarajiwa kumalizika June 27 mwaka huu.

 Mabadiliko hayo yanayogusa ratiba ya kuanza na kuahirishwa kwa vikao kila vinapoketi kuanzia hii leo, inaweza kuwa mwiba kwa wabunge wasioweza kutumia muda ipasavyo, kufuatia kupunguzwa dakika za kuchangia huku Siku ya Jumamosi ikitajwa kama siku rasmi ya mkutano tofauti na awali.

 Akitangaza mabadiliko hayo Bungeni Mjini Dodoma, Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge JOHN JOEL, amesema Kamati ya Uongozi imefikia makubalino hayo ili kufidia muda uliopotea na hatimaye bajeti ipitishwe na kuanza kutumika ifikapo Julai Mosi mwaka huu.

Baadhi ya Wabunge kama ilivyo kwa baadhi ya waandishi wa habari tayari wako mjini DODOMA kwa ajili ya kujisajili.
 Bunge hilo limeanza kuanza vikao vyake leo na mabadiliko hayo ya kanuni za Bunge pia yanatoa fursa kwa kila Wizara kuwasilisha Bajeti ya Makadirio ya Mapato na Matumizi yake kwa kipindi cha siku moja tu na muda utaongezwa mara itakapotokea dharura.

No comments:

Post a Comment