Friday, May 2, 2014

BADO KUNA CHANGAMOTO KWA WANAWAKE WAKIWEMO WAJANE KUFUATILIA NA KUTUMIA FURSA ZILIZOPO



Imeelezwa kuwa wanawake wakiwemo wajane ni miongoni mwa makundi ambayo yamekuwa yakiangaliwa na jamii, katika kuhakikisha yanapata fursa mbalimbali zinazojitokeza, huku kukiwa na changamoto ya makundi hayo kutojitambua katika kufuatilia na kuzitumia fursa hizo.
Hali hiyo inachangiwa na wanawake wajane walio wengi kujiona wanyonge katika jamii, lakini kupitia mashirika mbalimbali ,vikundi na serikali kwa ujumla, jitihada mbalimbali zimefanywa ikiwemo kutoa elimu ili kuhakikisha kundi hilo linapata fursa sawa hasa katika upatikanaji wa mikopo.
Akizungumza  Afisa Mtendaji wa kata ya uwanja wa Taifa Manispaa ya Morogoro Bi. ANNA KOBERO amesema, kwa kipindi kilichopita kina mama wa kata hiyo wamekuwa na tatizo la kupata mikopo,  lakini tangu kuanzishwa kwa vikundi vya kuweka na kukopa, kina mama wengi wameweza  kujikwamua kiuchumi na kukabiliana  na umaskini na unyanyasaji wa kipato.

Bw. SALUM KURUGE na Bi. ZAWADI CHANZI ni baadhi ya wanachama wa kikundi cha UMOJA VICOBA cha kata  ya Uwanja wa Taifa, ambao wamesema kupitia kikundi hicho, kujikopesha wao kwa wao imekuwa ni faida kubwa.
Kikundi cha Umoja Group cha kata ya Uwanja wa taifa manispaa ya Morogoro kilianzishwa mnamo mwaka elfumbili na kumi na tatu na kina wanachama thelathini.
mwisho

No comments:

Post a Comment