![]() |
KATIBU MKUU WA CCM ABDULRAHMAN KINANA AKIWAHUTUBIA WANANCHI WA KATA YA ROYA WILAYA YA UYUI MKOANI TABORA |
Imeelezwa kuwa
ongezeko la idadi ya vifo vya akina mama wajawazito na watoto walio chini ya
umri wa miaka 5 limezidi kushika kasi, hususani katika maeneo ambayo
hayafikiwi kiurahisi kutokana na miundo mbinu mibovu ya barabara na usafiri.
Kwa Tanzania hali
hiyo imebainika katika kata ya ROYA wilaya ya UYUI mkoani TABORA, ambako
wajawazito na watoto wadogo hawajawahi kupata chanjo, za kujikinga na
maradhi ya aina mbalimbali kwa zaidi ya miaka mitano.
Wananchi wa Kata
hiyo wakizungumza mbele ya Katibu mkuu wa chama cha Mapinduzi CCM, komredi
ABDULRAHMAN KINANA, wamedai hali hiyo imesababishwa na kukosekana kwa Jokofu la
kuhifadhia dawa katika Zahanati ya kata hiyo.
Mara baada ya
malalamiko hayo kutoka kwa wakazi wa kata hiyo, ikamlazimu katibu mkuu huyo wa
CCM komredi KINANA kumtaka mbunge wa Jimbo hilo ATHUMANI MFUTAKAMBA, kujibu
baadhi ya tuhuma hizo ingawa wananchi walionekana kutoridhishwa na majibu yake.
Hata hivyo
kero hizo hazikuanzia hapo, ambapo awali katibu mkuu huyo alipofika katika kata
ya MIYENZE wanachi katika eneo hilo ambao ni Jamii ya wafugaji wamelalamikia
vitendo vya kikatili vinavyofanywa na askari wanyamapori vya kuua mifugo yao na
kisha kuwakamata wamiliki wake.
Kufuatia
majibizano hayo Katibu mkuu wa CCM kwa mara nyingine tena ikamlazimu kuingilia
kati na kutoa maelezo ya kina huku akiahidi kuifuatilia kero hiyo na kuitafutia
ufumbuzi wa kudumu kulingana na mamlaka aliyopewa.
Wilaya ya
Uyui kwa sasa ina jumla ya wakazi wanaofikia 393,789, huku ikiwa na ongezeko la
idadi ya watu la wastani wa asilimia 4.8 kwa mwaka.
No comments:
Post a Comment