Wednesday, May 7, 2014

ZAIDI YA WANANCHI 200 WAFANYA MAOMBI KWENYE ENEO LILITOKEA VIFO VYA WATU 19 KWA AJALI MKOANI SINGIDA

ZAIDI ya wananchi 200 wa Kijiji cha Utaho jana wamefanya maombi kwenye eneo la ajali lililosababisha vifo vya watu 19, baada ya kugongwa na basi la Sumry, barabara kuu ya Singida-Dodoma.
Katika ibada hiyo, Wananchi wakiongozwa na viongozi wao wa dini Padri Felix Mange, mchungaji wa kanisa la Pentekoste Francis Pius na imamu wa kijiji hicho Haruna Senga wameiasa jamii kuchukua tahadhari wanapotumia barabara hiyo.Baada ya maombi hayo baadhi ya wakazi wa mji wa singida wameeleza kusikitishwa na ajali hiyo na wameiomba jamii kuendelea kuwafariji wale wote waliopoteza ndugu zao.
April 28 mwaka huu watu 19 walipoteza maisha wakiwemo askari polisi wanne,viongozi watatu wa kijiji na wengine wanane kujeruhiwa, baada ya kugongwa na basi la Sumry kwenye eneo la Utaho, Mkoani Singida.

No comments:

Post a Comment