Wednesday, May 7, 2014

MONICA LEWINSKY AMREKEBISHA BEYONCE KWENYE MASHAIRI YAKE YA WIMBO WA "PARTITION"



MONICA LEWINSKY

Wakati Beyonce amewaacha watu midomo wazi na albam yake ya mwaka jana, lakini mashairi yaliyoongelewa sana ni ya wimbo wa “Partition”  wakati mwanamuziki huyo alipoimba kuhusu mahusiano ya kimapenzi kati ya Bill Clinton rais wa zamani wa Marekani na Monica Lewinsky. Kuna mstari ulisema “Oh he is so horny, yeah he want to F word” aliimba Beyonce “He popped all my buttons and ripped my blouse /He Monica Lewinsky-ed all on my gown”. Aliongeza Beyonce kwenye wimbo huo.

 Katika mahojiano ya Vanity Fair “Shame and Survival” Lewinsky alimsahihisha Beyonce katika wimbo  huo kwamba alichokisema ni kwa mtu kufika kileleni kwenye gauni la mpenzi wake. “Ahsante, Beyonce” alisema Monica Lewinsky. Beyonce alisema “he Monica Lewinsky-ed” lakini alimaanisha “Bill Clinton did all on my gown” akasema “ He Monica Lewinskyd-ed all on my gown .

Karibu milongo miwili baada ya story hiyo kugonga sana vichwa vya habari Monica Lewinsky amebaki kuwa katika utamaduni wa muziki, Eminem alishakumbushia kwenye wimbo wake wa “Rap God” , Kanye West, Kid Cudi, Raekwon na Migos wote hao wamemtaja Monica kwenye nyimbo zao.
Akiwa na miaka 40 sasa Lewinsky anatokea akiwa msafi kuhusu mambo yaliyotokea zamani. Kwenye mahojiano alisema kweli anajutia mahusiano yake ya kimapenzi na Clinton. “Ni muda wa kuacha kuyaleta mambo ya nyuma sasa na ya watu wengine pia” alisema Monica Lewinsky. “Najitahidi kuweka mambo kuwa na utofauti wa mwisho wa story yangu, hatimaye nimeamua  kutazama tofauti juu ya story yangu ya nyuma  kwa hiyo naweza kufanya story yangu kuwa kitu ambacho ni muhimu, itanigharimu? Nitafahamu muda si mrefu" alisema.

 Mwaka 2014 mambo ya nyuma ya Monica Lewinsky bado yanamsumbua na kumuharibia pale anapokutana na  waajiri na kazi muhimu katika maisha yake. Kwa sababu waajiri wengine wanaangali masuala yake ya nyuma. “Nimekuwa sijisikii vizuri kabisa na hali hiyo kiasi fulani, nilikuwa sawa kwa sababu zisizo sawa” alisema Monica. 

Waajiri wengine wanamwambia kazi zile ambazo zitahitaji waandishi wa habari na akiwepo lazima watakumbushia kile kilichowahi kutokea katika maisha yake na hivyo katika masuala ya bidhaa inakuwa mbaya.

No comments:

Post a Comment