Saturday, May 17, 2014

ARSENALA YATOA UKAME WA MIAKA NANE BILA KIKOMBE YATWAA FA CUP

Baada ya miaka nane kupita bila Arsenal (The Gunners) kupata kikombe chochote, Leo hii Jumamosi 17  Mei  2014 wamefanikiwa kuchukua kikombe cha ubingwa wa FA kwa kuicharaza 3 – 2 Hull City katika mchezo uliokuwa mkali sana na wa kusisimua huku timu zote zikipelekeshana. 
Hull City ndio waliokuwa wa kwanza kuliona lango la Arsenal mapema kabisa katika dakika ya 4  kwa goli lililofungwa na Chester na dakika nne baadae katika dakika ya nane Davies aliipatia Hull City goli la pili. 
Goli la Kwanza la Arsenal lililorudisha matumaini lilifungwa katika dakika ya 17 na Carzola na mpaka inafika mapumziko ilikuwa Arsenal 1, Hull city 2. Katika kipindi cha pili dakika ya 71 Koscielny aliwainua mashabiki wa Arsenal baada ya kupachika goli wavumi. 
Dakika za kawaida zilimalizika zikaongezwa nyingine 30 na dakika 15 ziliisha bila timu yeyote kuliona lango la mwenzake. Katika kipindi cha pili katika muda wa nyongeza dakika ya 109 Ramsey alipachika goli zuri lilipea jina la Arsenal classic goal of the match baada ya kupewa pasi kwa kisigino na bila kutuliza Ramsey akanyoosha golini na kuiandikia Arsenal goli la 3 na ndilo lililowapa ushindi wa FA 2014. Imekuwa ni furaha kwa mashabikiwa Arsenal, kocha na wachezaji kwani ni muda mrefu miaka nane Arsenal hakushinda kombe lolote.

No comments:

Post a Comment