Tuesday, May 6, 2014

UKOSEFU WA ELIMU YA MAHESABU YA KISASA NI KIKWAZO CHA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI NYINGI NCHINI



Ukosefu wa elimu  ya mahesabu ya kisasa  juu ya ufungaji, uwasilishaji na utoaji taarifa za fedha  kwa halmashauri nyingi hapa nchini  inaelezwa kuwa kiwazo kwa halmashauri hizo kufikia malengo ikiwa ni pamoja na kupata hati chafu. 
 Mtaalamu wa masuala ya Fedha kutoka  kampuni ya Better Business Consultant   ya Jijiji Dar es salaam PEACE LUMELEZI,amebainisha hayo wakati akitoa mafunzo maalumu juu ya  ufungaji wa mahesabu kwa wahasibu wa serikali kutoka halmashauri za wilaya ya Kigoma  na kuongeza kuwa hali hiyo inakwamisha juhudi za kujiletea maendeleo katika baadhi ya halmashauri nchini.
  
Mpaka sasa zaidi ya watu 600 nchini kutoka Taasisi za serikali na binafsi wamekwisha nufaika na mafunzo hayo yanayolenga kuongeza kasi ya utendaji kazi kwa wahasibu.

No comments:

Post a Comment