Monday, May 19, 2014

UHABA WA WAUGUZI NCHINI UNASABAISHA WAUGUZI KUHUDUMIA WAGONJWA WENGI

Uhaba wa wauguzi nchini unasababisha wauguzi kuhudumia wagonjwa wengi kinyume na mwongozo wa shirika la afya duniani unaoelekeza muuguzi mmoja kuhudumia wagonjwa kati ya sita hadi wanane kwa siku.
Hali hiyo imejitokeza pia katika wilaya ya Momba mkoani Mbeya ambapo muuguzi mmoja anahudumia wastan wa wagonjwa 30 hadi 40 kwa siku.
Akisoma risala kwa niaba ya wauguzi,muuguzi DORIS JAPHET amesema tatizo la uhaba wa wauguzi linapelekea wafanye kazi kupita uwezo wao hali  inayosababisha kutoa huduma chini ya kiwango.
Nao baadhi ya wadau wa afya wilayani momba wamesema mbali na tatizo la uhaba wa wauguzi, pia vituo vya kutolea huduma za afya havitoshelezi.

No comments:

Post a Comment