Thursday, May 29, 2014

Imeelezwa Kuwa Maambukizi Ya Virusi Vya Ukimwi Yamepungua Nchini

Imeelezwa kuwa maambukizi ya virusi vya UKIMWI nchini yamepungua kutoka asilimia 5.7 mwaka 2008, na kufikia asilimia 5.1 kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa Machi  2013, huku Pemba ikiwa na maambukizi madogo ambayo ni kati ya asilimia 0.1 na 0.4.
Waziri wa Nchi, Sera, Uratibu na Bunge WILLIAM LUKUVI ameliambia Bunge, wakati akijibu swali la mbunge wa Wete MBAROUK SALIM ALI, kuwa mikoa mingi yenye maambukizi makubwa haifanyi tohara kwa wanaume ukiwemo mkoa wa Njombe wenye asilimia 14.8, Iringa asilimia 9.1, Mbeya asilimia 9, Shinyanga asilimia 7.4, Ruvuma asilimia 7, Dar es Salaam asilimia 6.9, Katavi asilimia 5.9 na mkoa wa Pwani asilimia 5.9.

No comments:

Post a Comment