Imeelezwa kuwa maambukizi ya virusi vya UKIMWI
nchini yamepungua kutoka asilimia 5.7 mwaka 2008, na kufikia asilimia 5.1 kwa
mujibu wa takwimu zilizotolewa Machi 2013, huku Pemba ikiwa na maambukizi
madogo ambayo ni kati ya asilimia 0.1 na 0.4.
Waziri wa Nchi, Sera, Uratibu na Bunge WILLIAM
LUKUVI ameliambia Bunge, wakati akijibu swali la mbunge wa Wete MBAROUK SALIM
ALI, kuwa mikoa mingi yenye maambukizi makubwa haifanyi tohara kwa wanaume
ukiwemo mkoa wa Njombe wenye asilimia 14.8, Iringa asilimia 9.1, Mbeya asilimia
9, Shinyanga asilimia 7.4, Ruvuma asilimia 7, Dar es Salaam asilimia 6.9,
Katavi asilimia 5.9 na mkoa wa Pwani asilimia 5.9.
No comments:
Post a Comment