Friday, May 2, 2014

PAMOJA NA NCHI NYINGI KUSAINI MKATABA WA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI BADO SHERIA NYINGI ZINAKINZANA NA MKATABA HUO



Mhadhiri mwandamizi wa shule ya uandishi wa habari Dk. Ayou Rioba

Pamoja na wakuu wa nchi nyingi duniani kusaini mkataba wa uhuru wa vyombo vya habari, bado sheria za nchi nyingi zinakinzana na mkataba huo,  ikiwemo sheria ya magazeti ya mwaka 1976 ambayo inatumika hapa nchini.
Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari, yanayofanyika kitaifa jijini Arusha, mhadhiri mwandamizi  wa shule ya uandishi wa habari Dk. AYOUB RIOBA  amesema, sekta ya habari imepiga hatua licha ya changamoto nyingi zinazoikabili.

Naye mwanahabari mwandamizi LEILA SHEHE amewataka waandishi wa habari kujitathmini katika uhuru huo, ili kuona  kama unatekelezwa hasa kwa kutoa habari kwa kuheshimu misingi yake.
Baadhi ya waadhishi wa habari  akiwemo mhadhiri mwandamizi wa chuo kikuu cha Iringa SIMON BEREGE, wameitaka serikali kuweka  sheria dhidi ya wanaotumia mitandao vibaya, ili kila mtu aweze kuitumia.
Mkutano huo wenye kaulimbiu ya ‘’uhuru wa vyombo vya habari kwa utawala bora na maendeleo’’ umewakutanisha waandishi wa habari kutoka ndani na nje ya nchi,  ambapo leo wamiliki wa vyombo vya habari,  wanatarajiwa kuungana nao katika kujadili changamoto mbalimbali.

No comments:

Post a Comment